Maksimo Muungamadini

Maksimo Muungamadini (Haspin, Siria, 580 hivi - Tsageri, leo nchini Georgia, 13 Agosti 662) alikuwa mmonaki padri maarufu kwa ari na teolojia yake.

Picha takatifu ya Mt. Maksimo kadiri ya mtindo wa Ukristo wa mashariki.
Picha takatifu ya Mt. Maksimo kadiri ya mtindo wa Ukristo wa mashariki.

Miaka 615-645 aliishi Karthago, leo nchini Tunisia.

Jina la pili aliongezewa kutokana na mateso yaliyompata kwa ajili ya imani sahihi dhidi ya waliokanusha utashi wa kiutu wa Yesu: chini ya kaisari Konstas II alikatwa mkono wa kulia na ulimi asiweze kuendelea kuitetea wala kwa maandishi wala kwa sauti.

Hatimaye alipelekwa uhamishoni pamoja na wanafunzi wake wawili wenye jina moja, Anastasi, na ndipo alipofariki[1].

Mtaguso wa tatu wa Konstantinopoli ulimpa ushindi baada ya kifo chake.

Tangu kale anaheshimiwa na Kanisa Katoliki, Waorthodoksi na wengineo kama mtakatifu na babu wa Kanisa.

Sikukuu yake inaadhimishwa tarehe 13 Agosti[2] au 21 Januari.

Tazama pia

hariri

Tanbihi

hariri

Marejeo

hariri
  • Vita ac certamen S. Maximi (PL 90,67-110): Wasifu rasmi kwa Kilatini.
  • P. Sherwood, St Maximus the Confessor. London, 1955
  • Jean-Claude Larchet, Saint Maxime Le Confesseur. Paris, 2003

Viungo vya nje

hariri
  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.